Watu 20 wauwawa Kenya katika shambulizi la jana usiku



TAKRIBAN watu 20 wameuawa katika shambulizi la pili la usiku katika pwani ya Kenya.
Kundi la wapiganaji la Al Shabaab limekiri kutekeleza shambulizi hilo la pili katika vijiji viwili zaidi na kusema wengi waliouawa ni maafisa wa polisi.
Wapiganaji hao walivamia vijiji viwili karibu na mji wa Mpeketoni, ambao ni eneo la mashambulizi ya kwanza yaliyosababisha mauaji ya watu 48.
Tukio hilo limetokea licha ya maafisa wengi wa polisi kupelekwa katika eneo hilo kufuatia mauaji hayo ya Jumapili.
Kwa mujibu wa BBC, wakazi wa eneo hilo wamelalamikia Serikali kwa kutowapa ulinzi baada ya shambulizi la kwanza na sasa wanaishi kwa hofu.
Serikali imesema wanamgambo wa Al Shabaab walikata mawasiliano ya simu katika eneo hilo kabla ya kutekeleza shambulizi hilo.
Wanamgambo hao wanaohusishwa na kundi la Al Qaeda wamesema wataendelea kufanya mashambulizi nchini Kenya ikiwa serikali haitaondoa wanajeshi wake nchini Somalia.
Shambulizi hilo la vijijini limeonekana kuwa mfumo mpya wa mashambulizi ambayo yamekuwa yakifanywa na Al Shabaab ambao mara nyingi wamekuwa wakilenga maeneo ya mijini hasa miji mikubwa.
Takriban watu 48 waliuawa katika mashambulizi yaliyofanyika usiku wa kuamkia Jumatatu huku watu wenye silaha wakishambulia hoteli na kituo cha polisi pamoja na kuteketeza magari.
Wakati huohuo, Rais wa Kenya, Uhuru Kenyatta, amesema mauaji yaliyofanywa katika mji wa Mpeketoni hayakufanywa na kundi la wapiganaji wa Kiislamu la Al Shabaab.
Kauli ya Rais Kenyatta inakuja kupitia televisheni siku moja baada ya kundi hilo kukiri kufanya mauaji yaliyotokea Mpeketoni Jumapili usiku.
Rais Kenyatta amesema kuna ushahidi kuonesha kuwa shambulizi hilo lilipangwa vyema na kwamba wanasiasa nao walihusika.

  • Digg
  • Del.icio.us
  • StumbleUpon
  • Reddit
  • RSS

Namna ya kuosha uso kwa gharama nafuu bila matumizi ya kemikali.



Usafishaji wa uso ni muhimu sana katika utunzaji wa ngozi aidha kwa mwanamke hata pia mwanaume ili kujihakikisha afya nzuri na muonekano mzuri,leo kupitia Maridadi Agency tutajifunza namna ya kusafisha uso pila kutumia kemikali ya aina yoyote .
na ni njia ambayo ni safi na salama kwa afya yako.

Mahitaji

  1. Maziwa ya mgando
  2. Mlozi na karoti
  3. Maji vuguvugu
  4. Limao
  5. Taulo laini au la pamba

   Njia


1. Chukua maziwa ya mgando na utumie kusafisha uso wako.
2. Scrub kwa kutumia mchanganyiko wa mlozi na karoti au mlozi wa jani la chai.
3. fanya toning na maji vuguvugu yaliyochanganywa na kipande cha limao na weak kidogo katika taulo la pamba na futa uso wako mahali pote kasoro penye tatizo.
4. Tumia ute mweupe ambao utakuwa umemwagia katika taulo lako na kujisugua taratibu.
5. Jisafishe na maji ya vuguvugu
6. Fanya toning tena kama ilivyokuwa katika hatua ya tatu juu
7. Ili kuondoa ukavu wa ngozi, kata matango na yabandike katika ngozi.

  • Digg
  • Del.icio.us
  • StumbleUpon
  • Reddit
  • RSS

Bomu lasadikika kulipuka siku ya jana Zanzibar na kuua mtu mmoja.


Mlipuko ambao unasadikika na watu wengi kuwa ni bomu lililotegwa kwa dhumuni maalumu limelipuka siku ya jana na kufanikiwa kukuua mtu mmoja huku akiwaacha watu watatu majeruhi.


Aliyefariki ni mmoja kati ya wahadhiri waliokuja kutoka Tanga na S waliojeruhiwa ni sheikh Hamad pamoja na Sheikh Kassim Mafuta ambae amepata majeraha kidogo.Majeruhi wote wamelazwa hospitali ya Mnazi Mmoja, Zanzibar.


  • Digg
  • Del.icio.us
  • StumbleUpon
  • Reddit
  • RSS

AIBU:BIBI aanguka jijini Mwanza baada ya kushushwa katika Ungo.












Bibi mmoja ambaye jina 
lake halikuweza kufahamika amekutwa katika mazingira ya kutatanisha jijini Mwanza yaliyojenga mitazamo tofauti kutokana na imani za watu wengi
Bibi huyo pindi alipokuwa akiojiwa na baadhi ya watu mbalimbali waliomzunguka alidai kuwa  ametokea mjini Bariadi na alishushwa na wenzake wanne waliokuwa katika safari zao usiku  ndani ya chombo chao cha asili maarufu kama Ungo baada ya kugombana kwa muda mrefu.
\
Bibi huyo alikuwa akionekana eneo maarufu hospitalini sekoutoure akiangaika kwa kuranda huku na kule,aidha mitazamo ya watu tofauti hasa kundi lililodai kuwa bibi huyo ni mwaka na kutaka kujichukulia sheria mkononi ya kutaka kumpiga mawe lilifuta hisia za chombo cha dola ambao walifika muda mchache na kuwatawanya watu wote waliokuwa wamemzunguka. 

Bibi akiwa mpweke baada ya kutawanywa watu wote waliomzunguka








  • Digg
  • Del.icio.us
  • StumbleUpon
  • Reddit
  • RSS

Mwanamuziki wa Injili Happy haukumiwa kifungo cha miezi mitatu.







Habari za Uhakika zilizopo mjini Mbeya zinasema kuwa Mwanamuziki wa Injili nchini Tanzania anayejulikana kwa jina la Happy Kamili anayetamba sana na wimbo wake "Mpango Wa Mungu" na "Jina Kubwa" amehukumiwa kifungo cha Miezi Mitatu Jela bila faini katika Mahakama Ya Mwanzo Mkoani humo kwa Kosa la Kusababisha ajali ya barabarani.






Kesi hiyo iliyokuwa imeanza kusikilizwa mwezi January Mwaka huu, siku ya jana imetolewa hukumu kwa Mwanamuziki huyo kupatikana na hatia ya kusababisha ajali kwa kugonga gari lingine kwa nyuma. Mwanamuziki huyo baada ya Kukiri kutenda kosa hilo mahakamani alipatikana na hatia ya Hakimu alitoa Hukumu ya Miezi Mitatu Jela pasipo kutoa Hukumu Mbadala ya Faini.


  • Digg
  • Del.icio.us
  • StumbleUpon
  • Reddit
  • RSS

Mwanza:Mtoto awa mfugo kama mbuzi kwa mganga wa kienyeji.





MATUKIO ya ukatili dhidi ya watoto, bado yameendelea kushika kasi kwenye maeneo mbalimbali nchini ambapo katika Mkoa wa Simiyu, mtoto mwenye umri wa miaka 17 (jina tunalihifadhi), mkazi wa Bariadi Mjini na mwanafunzi wa Shule ya Msingi Bariadi, amejikuta akifungwa kamba mikononi na miguuni kwa miezi minne nyumbani kwa mganga wa kienyeji.


Mganga huyo amefahamika kwa jina la Mdeli Msanja ambaye aliamua kufanya ukatili huo baada ya wazazi wa mtoto huyo ambaye anamatatizo ya akili, kushindwa kumlipa pesa za matibabu. Akizungumzia tukio hilo, Kamanda wa Polisi mkoani humo, Charles Mkumbo, alisema wazazi wa mtoto huyo walikubaliana na mganga huyo kumlipa sh. 260,000 kama mtoto wao atapatiwa matibabu na kupona.

“Pamoja na wazazi kukubaliana na mganga husika, hali ya mtoto haikuweza kubadilika wala kupata unafuu hivyo waliomba kumchukua mtoto wao kitendo ambacho kilipingwa na mganga kwa madai ya kutolipwa pesa zake ambazo walikubaliana,” alisema.


Alisema mganga huyo aliamua kumchukua mtoto huyo na kumfungia chumbani kwake kwa kamba miguuni na mikononi kwa kipindi cha miezi minne akidai pesa zake na kuwapa wakati mgumu wazazi wake. Kutokana na msimamo wa mganga huyo, mama mzazi wa mtoto huyo Malita James (46), alilazimika kwenda kutoa taarifa Kituo cha Polisi Bariadi kuhusu mateso anayoyapata mwanaye kwa mganga.

“Polisi walishirikiana na Dawati la Jinsia kufanya uchunguzi wa tukio hili na walipofika kwa mganga, walimkuta akiwa amemfunga kamba miguuni na mikononi,” alisema Kamanda Mkumbo.

Aliongeza kuwa, polisi walimkamata mganga huyo ambaye hakuwa na kibali cha kutoa tiba za asili, pia alikamatwa na nyara za Serikali ambazo ni pembe moja ya swala na mikia miwili ya nyumbu ambapo uchunguzi ukikamilika atafikishwa mahakamani.

  • Digg
  • Del.icio.us
  • StumbleUpon
  • Reddit
  • RSS

Hatari ya mapenzi ya Facebook




Dada mmoja alikutana na kijana mmoja kwa njia ya facebook na wakapendana hapa mtandaoni.
Baada ya kuchati kwa muda mrefu wakaamua waende kuonana na hatimaye wakaona na binti kukaribishwa katika chumba alichopanga kijana huyo.
Alipofika akaanza kuhisi kuwa amefanya maamuzi yasiyo sahihi kwenda pale kwani chumba kilinuka harufu ya pombe na bangi na pia kulikuwa na vijana wengine wapatao wanne wakiwa wamelewa pale.
wakamwingilia kinguvu dada yule na kisha baada ya kugundua kapoteza fahamu wakamtupa nje karibu na barabara na dada alipopata fahamu kwa aibu akaondoka na hakumwambia mtu na kukaa kimya.
Miezi michache baadae akagundua kuwa ni mjamzito na kwa sheria za ile nchi akatakiwa kufukuzwa katika ile jamii kwani amefanya kosa la kuiabisha jamii kupata ujauzito bila muda wake muafaka kufikia.
Siku chache baadae ikaja onekana maiti yake ikiwa pembeni ya mji ule katika nyumba moja akiwa na karatasi mkononi iliyoandikwa:
" Kwa wadogo zangu miliobaki, mitandao ya kijamii ina faida kubwa na hasa zake pia... kamwe msiwe wepesi wa kufanya maamuzi na kuja kuwa wahanga wa matatizo niliyokumbana nayo mimi dada yenu.... Nawapenda sana"
Sala kwa ajili yako
Mitandao ya kijamii itakupa marafiki watao kupanua mawazo ya kuziboresha kazi zako na sio watakao kuharibia kazi zako na maisha yako pia.
Kila rafiki atakuwa hazina ya mafanikio yako nawe utapata busara na hekima ya kuwatambua marafiki feki na wale wenye nia njema

  • Digg
  • Del.icio.us
  • StumbleUpon
  • Reddit
  • RSS